Balozi wa Tanzania nchini Brazil Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Brazil Mhe. Michel Temer, Tarehe 26 Juni, 2017. Rais Temer alisifu jitihada za Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kupigana na umasikini na kuleta maendeleo kwa wananchi. Brazil imeihakikishia kuunga mkono juhudi za Serikali  ya Tanzania katika kufanikisha miradi mbalimbali ya ushirikiano.